head>

News & Official Reports

Complete updates from ZANAB Zanzibar

April 30, 2026

MKUTANO WA KUANZISHA KAMATI YA KUENDESHA MRADI,MAALUM KWA KUBORESHA ELIMU MJUMUISHO KWA WATU WASIOONA NA WENYE UALBINO

Tarehe 16 April 2026 ZANAB ilifanya mkutano wa kuanzisha kamati ya kuendesha mradi maalum kwa kuboresha elimu mjumuisho kwa watu wasioona na wenye ualbino Wilaya ya Magharibi "B"Fuoni
Mkutano huo ulifanyika ofisi ya elimu Fuoni uliwakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo masheha na watu wenye ulemavu
Jumuiya ya wasioona zanzibar(ZANAB) imekuwa inatekeleza mradi wa upatikanaji wa huduma bora za afya,elimu jumuishi na ustawi wa kiuchumi kwa watu wasioona na wenye ualbino.Huu ni mradi wa miaka mitatu ulioanza mwaka huu 2026 na kumalizika 2028.Mradi unafadhiliwa na shirika la MyRight kupitia washirika wao kutoka chama cha wasioona cha Swiden(SRF).
April 30, 2026

ZANAB YAHIMIZA UPATIKANAJI WA ELIMU BORA JUMUISHI,HUDUMA ZA AFYA NA USTAWI WA UCHUMI KWA WATU WASIOONA NA WENYE UALBINO

Tarehe 21 April 2026 ZANAB ilifanya mkutano wa kuanzisha kamati ya kuendesha mradi maalum kwa kuboresha elimu mjumuisho kwa watu wasioona na wenye ualbino Wilaya ya Chake Chake Pemba Ofisi ya ZANAB vitongoji
Jamii yahimizwa kutowafungia ndani watu wasioona na wenye ualbino bali watolewe na kuandikishwa skuli.Haya aliyasema mratibu wa ZANAB Bwana Adil Mohamed Ali katika mikutano tofauti yaliyofanyika katika ofisi ya elimu wilaya ya magharibi “B” Fuoni Unguja tarehe 16/04/2026 na tarehe 21/04/2026 katika ofisi ya ZANAB vitongoji wilaya ya Chakechake Pemba.
April 26, 2026

CALL FOR CONSULTANT

ZANAB (Zanzibar National Association of the Blind) through the CADIR Project invites qualified and experienced consultants to apply for consultancy services.

🔹 Scope of Work:
• Review ZANAB HR Manual Policy
• Review ZANAB Whistle Blowing Policy
• Review ZANAB Code of Conduct
• Develop ZANAB Sexual Harassment Policy
• Facilitate Board Governance Training
• Review ZANAB Risk Management Policy
• Develop ZANAB Financial Sustainability Strategy

🔹 Location: Zanzibar

🔹 Requirements:
Applicants should have experience in organizational governance, policy development, training facilitation, and strategic planning. Experience in disability inclusion will be an added advantage.

How to Apply:
Interested candidates should submit:
• Curriculum Vitae (CV)
• Application Letter
• Technical Proposal
• Financial Proposal

Send your application to: wasioona@gmail.com
Deadline: 5th May 2026
Women and persons with disabilities are highly encouraged to apply.
April 23, 2026

MKUTANO WA KUJENGA UELEWA KUHUSU CBID WILAYA YA KUSINI UNGUJA

Tarehe 22 Aprili 2026,ZANAB kupitia mradi wa CADIR lilifanya mkutano wa kujenga uelewa wa CBID katika Wilaya ya Kusini, Unguja.

Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa Kituo cha Walimu Kitogani na uliwakutanisha wadau mbalimbali wakiwemo masheha, watu wenye ulemavu, pamoja na maafisa wa ngazi ya wilaya wakiwemo Afisa Elimu, Afisa wa Watu Wenye Ulemavu na Afisa wa Kituo cha Afya. Aidha, viongozi wa ZANAB walishiriki kikamilifu katika mjadala huo.

Lengo la mkutano lilikuwa ni kuongeza uelewa kuhusu CBID na kuimarisha ushirikiano kati ya wadau mbalimbali ili kuhakikisha utekelezaji wenye ufanisi wa shughuli za maendeleo jumuishi katika jamii.
April 16, 2026

ZANAB ANNUAL REPORT

This Activity Implementation Report of the Zanzibar National Association of the Blind (ZANAB) provides a comprehensive account
of activities implemented during the period from January to December 2025. The report is prepared for presentation to the ZANAB
National Executive Council, development partners, and the Government, for the purpose of accountability, performance assessment,
and planning for the implementation of activities in the subsequent year.